Ibrahim Ajib aanza mazoezi na Yanga SC

Ibrahim Ajib aanza mazoezi na Yanga SC


Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC imeanza kuwafua wachezaji wake kwa mazoezi mepesi mepesi kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi kuu na mashindano ya kimataifa kwenye uwanja wa uhuru Jijini Dar es Salaam.


Wachezaji wa klabu ya Yanga wakiwa katika mazoezi

Kocha Mkuu wa klabu hiyo raia wa Zambia, George Lwandamina ameonekana akikiandaa kikosi hicho kipya kikiwa na wachezaji wapya waliosajiliwa katika dirisha hili la usajili akiwepo mchezaji aliyetokea Simba, Ibrahim Ajib na Abdallah Haji Shaibu ‘Ninja’

Katika hatua nyingine timu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Karia Koo imesajili mlinda mlango mpya raia wa Cameroon, Youthe Rostand kwa mkataba wa miaka miwili African Lyon hivi karibuni ili aweze kusaidiana na Beno Kakolanya baada ya zile tetesi zikidai Ally Mustafa kuondoka kwenye kikosi hicho cha Jangwani na amekuwa akihusishwa kujiunga na Singida.

Post a Comment

0 Comments