McGregor amlaumu refa kumaliza pambano mapema ‘Angeacha hadi mwisho’

McGregor amlaumu refa kumaliza pambano mapema ‘Angeacha hadi mwisho’

Baada ya kupokea kichapo leo asubuhi Mwanamasumbwi, Conor McGregor amedai kuwa refa aliyechezesha pambano hilo, Robert Byrd alifanya makosa kusimamisha mchezo huo dhidi ya Floyd Mayweather katika raundi ya kumi.

Mayweather akimshindilia masumbwi McGregor

Bingwa huyo wa UFC alipigwa katika pambano lake la kwanza la kulipwa huku Floyd Mayweather akiimarisha rekodi yake ya kutopoteza pambano lolote kwa michezo 50 aliyocheza.

‘‘Niliona pambano tangia mwanzo tulikuwa sawa ingawaje niliyumba kidogo mwishoni kwani nilianza kuchoka, madhani Refa angeacha pambano liendelee na kumruhusu Mayweather kuniangusha, nilikuwa najua nilichokuwa nikifanya raundi mbili za mwisho nilitaka nione kama anaweza kuniangusha, Nilidhani ilikuwa mapema mno kwa refa kusimamisha pambano, Nilitaka kuendelea hadi raundi ya mwisho”,amesema McGregor kwenye mkutano na waandishi wa habari mapema baada ya kumalizika kwa pambano.

Hata hivyo, McGregor amesema atarudi kuendelea na mchezo wake wa UFC akikiri wazi kuwa mchezo wa Boxing ni mgumu.

Post a Comment

0 Comments