Ijue Sababu Kwanini Wachawi Wakiingia Nyumbani Kwa Mtu Kuwanga Huwa Hawaibi Pesa.

Ijue Sababu Kwanini Wachawi Wakiingia Nyumbani Kwa Mtu Kuwanga Huwa Hawaibi Pesa.



Wachawi wakiingia nyumbani kwa mtu kuwanga huwa hawachukui hata senti tano hata kama watakuta kuna mamilioni ya pesa yamezagaa kwenye kitanda au kwenye kabati. 



Nyuma ya jambo hili kuna siri moja nzito sana ambayo inahusiana na maisha ya kila mwanadamu. Je unataka kuijuia siri hiyo ?


Basi siri ya jambo hili ni moja tu nayo ni kwamba wachawi wanapokuwa wanataka kuiba kitu cha mtu kwa kutumia uchawi huwa WANAIBA CHANZO.


Chanzo cha mtu kuwa na pesa au kuwa tajiri ni NYOTA yake. Nyota yako wewe ndio imekufanya upate pesa na mali ulizo nazo.


Wachawi wakitaka kukuibia utajiri wako hawakuibii pesa zako bali wanakuibia nyota yako kwa sababu ndani ya nyota yako ndio kuna utajiri wako.


Vile vile wachawi wakitaka kuharibu , kushusha au kuua mafanikio ya mtu huwa WANAUA AU KUHARIBU CHANZO na chanzo cha mafanikio ya mtu ni nyota yake.


Kwa hiyo wanachokifanya wachawi ni kuharibu na kuua nyota yako. Nyota yako ikiharibika basi mambo yako mengine yataharibika pia.


Nyota yako ikifa basi mambo mengine yote yatakufa pia. Kwa ufupi maisha unayo ishi ni tafsiri ya mambo yanayo endelea katika nyota yako.


Ikumbukwe pia kuwa nyota ya mwanadamu inaundwa na mambo tisa na moja kati ya mambo tisa yanayo unda nyota ya mwanadamu ni pamoja na utajiri.


Nadhani mpaka hapo umeshaelewa kwanini wachawi wakiingia nyumbani kwa mtu kuroga au kuwanga huwa hawawezi kuiba wala kuchukua pesa au kito chochote cha thamani ndani ya nyumba waliyo ingia kuwanga.


MAKALA HAYA YAMEANDALIWA NA DOKTA. MUNGWA KABILI.ANAPATIKANA KWA SIMU NAMBA 0744 000 473.

Post a Comment

0 Comments