BREAKING NEWSS:BALOZI MWAPACHU ANG’ATUKA UJUMBE WA BODI YA ACACIA

BREAKING NEWSS:BALOZI MWAPACHU ANG’ATUKA UJUMBE WA BODI YA ACACIA



Balozi Juma Mwapachu

Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni ya uchimbaji ya Acacia, Balozi Juma Mwapachu amestaafu nafasi hiyo baada ya kuitumikia kwa vipindi viwili.
Mwapachu amechukua uamuzi huo leo, Julai 13 baada ya muhula wake wa pili wa miaka mitatu mitatu wa ujumbe wa bodi hiyo, kumalizika.
Taarifa iliyotumwa leo na Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Acacia imeeleza kuwa inamshukuru Balozi Mwapachu kwa utendaji wake na ushirikiano wake wote alipokuwa mjumbe.
“Tunamtakia maisha mema,” imesema taarifa hiyo.
Kutokana na mabadiliko hayo, Bodi ya Acacia itabaki na wajumbe saba, wakiwamo wanne wakurugenzi na wasio wakurugenzi.

Post a Comment

0 Comments