Magufuli ampokea Museveni Chongoleani

Magufuli ampokea Museveni Chongoleani


Rais wa John Magufuli na Rais wa Uganda Yoweri Museveni wamewasili kijini Chongoleani mkoani tanga kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa bomba la kusafirisha mafura ghafi.
Bomba hilo litatumika kusafirisha mafuta hayo kutoka Hoima nchini Uganda ambako yatachimbwa hadi bandari ya Tanga.
Pamoja na marais hao wawili, shughuli hiyo pia inahudfhuriwa na viongozi wengine wa juu akiwamo makamu wa rais, Samia Suluhu hassan na waziri Mkuu, kassim majaliwa.
Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akcson pia anahudhuria shughuli hiyo sambamba na Waziri wa Uchukuzi Mawasiliano na Ujenzi, Profesa Makame Mbarawa pamoja na Spika wa zamani wa Bunge, Anne Makinda.
Baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Chongoleano, marais hao wawili wanatarajiwa pia kufanya hivyo huko Hoima katika tarehe itakayotangazwa baadaye.

Post a Comment

0 Comments