Shigella aanza kutafuta ardhi ya makazi wa wawekezaji

Shigella aanza kutafuta ardhi ya makazi wa wawekezaji


Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella amesema uongozi wa mkoa huo tayari umeshaanza kuandaa mazingira ya kusaidia upatikanaji wa maeneo ya ardhi kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya wawekezaji wakati wa utekelezaji wa mradi wa bomba la mafutaghafi kutoka Hoima, Uganda, hadi bandari ya Tanga.


Shigella amesema mbali na hatua hiyo, pia imewahakikishia wawekezaji na Watanzania kupata maeneo ya ofisi zitakazohusika kwenye utekelezaji wa mradi huo.


Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi wakati wa sherehe za uwekaji jiwe la msingi la mradi huo zinazoendelea katika kijiji cha Chongoleani, mkoani Tanga. Katika sherehe hizo, Rais John Magufuli na mgeni wake, Yoweri Mseveni ambaye ni Rais wa Uganda wataweka jiwe hilo ikiwa ni hatua ya ufunguzi wa mradi


"Tumeshaanza kuhimiza watoto wetu waende vyuoni ili wapate ujuzi utakaowasaidia kuajiriwa wakati wa mradi, fursa zilizopo zitasaidia kuinua kipato cha wakazi na kupunguza umasikini,kwa hiyo mheshimiwa Rais wakati wa Tanga wanaomba useme neno moja tu na roho yao itapona,"alisema.

Post a Comment

0 Comments