Marekani yazuia mali za Maduro

Marekani yazuia mali za Maduro


Muda mfupi baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi uliokumbwa na mgogoro Venezuela, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imetoa taarifa kutishia kumchukulia kiongozi wa taifa hilo hatua nzito na za haraka.

Kwa kuanzia imezuia mali zote anazomiliki Maduro nchini Marekani na Waziri wa Fedha Marekani, Steven Mnuchin, amemtaja Maduro kuwa dikteta.

"Uchaguzi unathibitisha Maduro ni dikteta asiyezingatia matakwa ya raia wa Venezuela," amesema katika taarifa yake.

Hii si mara ya kwanza kwa marekani kuchukuwa hatua dhidi ya viongozi wa serikali hiyo , huku viongozi wakuu 13 wa utawala wa Maduro wakilengwa kwa vikwazo kama hivyo vilivyotangazwa wiki iliopita.


Post a Comment

0 Comments