Jux na Vanessa Wamewapa Changamoto Diamond na Wasafi Festival

Jux na Vanessa Wamewapa Changamoto Diamond na Wasafi Festival



Wasanii wa muziki wa Bongo fleva Juma Jux na Mpenzi wake Vanessa Mdee wamewapa changamoto kubwa Diamond na timu nzima ya WCB.

Jux na Vanessa ambao wamemaliza tour yao ya ‘In Love and Money’ ambayo imefanya vizuri sana kuliko ilivyotegemewa wameonekana kuwapa changamoto WCB ambao nao wametangaza kuja na Tour yao ya Wasafi Festival.

Babu Tale ambaye ni Meneja wa Diamond na mratibu wa Wasafi Festival amesema , kwamba mafanikio makubwa na tamasha hilo ni changamoto kwa tamasha la Wasafi Festival ambayo litaanza kutimua vumbi miezi michache ijayo.
Katika Show ya Aug 4, 2018 Dar es salaam, kila msanii aliuwa kwa show kali na stage na mashabiki walijitokeza kuenjoy, show ilikua na mizuka ya hali ya juu na surprise za kutosha kutoka kwa Mirror, Lady Jaydee na Chid Benz.

List ya Wasanii walioperform ilikuwa ya kizazi sana, Weusi, MOCO, Navykenzo, Mimi Mars, Kreest wa Gabon, Jojo wa Gabon, Marioo, Ben Pol, Maua Sama, Brian Simba, na wengine kibao na HOST wa Show nzima alikuwa Presenter mkali kutoka show ya The Playlist, Times FM - Lil Ommy, THE MVP, Halfman, Half Amazing.

Post a Comment

0 Comments