Liverpool yalipiza kisasi kwa Leicester, yaipiga 3-2

Liverpool yalipiza kisasi kwa Leicester, yaipiga 3-2


Nyota Mbrazil, Philippe Coutinho (kulia) akishangilia na mchezaji mwenzake, Alberto Moreno baada ya kuifungia Liverpool bao la pili dakika ya 23 katika ushindi wa 3-2 dhidi ya wenyeji, Leicester City Uwanja wa King Power. Mabao mengine ya Liverpool yamefungwa na Mohamed Salah dakika ya 15 na Jordan Henderson dakika ya 68, wakati ya Leicester yamefungwa na Shinji Okazaki dakika ya 45 na ushei na Jamie Vardy dakika ya 69, ambaye dakika ya 73 mkwaju wake wa penalti uliokolewa na kipa Simon Mignolet kufuatia yeye mwenyewe kuangushwa na mlinda mlango huyo.

Post a Comment

0 Comments